Ujumbe uliopewa Medjugorje mnamo Septemba 25, 2017

“Watoto wapendwa! Leo nakualika uwe mkarimu katika kujikana, kufunga na kuwaombea wale wote walio katika majaribu, na ni ndugu zako. Kwa namna ya pekee ninawaomba muwaombee mapadre na watu wote waliowekwa wakfu ili wampende Yesu kwa bidii zaidi, ili Roho Mtakatifu aijaze mioyo yao kwa furaha, ili watoe ushuhuda kwa Mbingu na mafumbo ya mbinguni. Nafsi nyingi zimo katika dhambi kwa sababu hakuna wanaojitoa mhanga na kuwaombea uongofu. Niko pamoja nanyi na ninawaombea ili mioyo yenu ijazwe na furaha. Asante kwa kuitikia wito wangu ”.